251. Mungu twakuimbia

1 Mungu twakuimbia,
tunasifu nguvu zako.
Tunakuangukia
kwa kuona mambo yako.
Ulivyokuwa kale
utakuwa milele.

2 Nchi zote na mbingu,
na majeshi yao yote,
wote wakuimbia.
Hata wingi wa malaika
wakusifu mbinguni
Ee Mungu mtakatifu.

3 Bwana wetu Mungu mkuu
mtakatifu mwenyezi,
u shujaa na Mwokozi.
Mbingu, viumbe, bahari
zimeumbwa na wewe,
zote zinakusifu.

4 Duniani popote
watu wako wakusifu,
ni wazee na watoto
wakuimbiao Baba,
wamsifuo Mwanao
na Roho Mtakatifu.

5 Bwana uturehemu,
utupe baraka yako.
Neema yako iwe kuu,
kwao wakuogopao.
Tunakutumaini,
hivi hatupotei.

Text Information
First Line: Mungu twakuimbia
Title: Mungu twakuimbia
German Title: Grosser Gott, wir loben dich
Author: Ignaz Franz, 1719-1790
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kumtambikia Mungu: Kumsifu na kumwomba Mungu
Notes: Sauti: Grosser Gott, wir loben dich, Asili: P. Ritter (?), Wien 1779, Posaunen Buch, Erster Band #247, Nyimbo za Kikristo #199
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us