252. Nakuimbia wewe Bwana

1 Nakuimbia wewe Bwana
hakuna mwingine kama wewe.
Nakuimbia nyimbo zangu,
unipe nguvu ya roho wako,
anifundishe nyimbo za sifa,
niziimbe kwa jina la Yesu.

2 Baba univute kwa Mwanao,
Mwanao anivute na kwako.
Mtakatifu uniongoze,
mawazo yangu yawe mazuri.
Amani yako ikae mwangu,
nikuimbie kwa furaha kuu.

3 Ukinisaidia hivi,
Bwanangu, nitaweza kuimba
kukusifu wewe vizuri
kwa roho na kwa kweli kila saa.
Maana Roho aniongoza
niimbe malaika waimbavyo.

4 Naomba nilivyofundishwa
na Roho wako, yakupendeze.
Nawe unasikia yote
sababu ya Mwana wako Yesu,
aliyenifanya mtoto wako
na mrithi wa ufalme wa mbingu.

5 Ni heri nikijua haya!
Naweza kukuomba vizuri:
Najua kila kitu chema
nitakachoomba nitapewa,
sababu kila kipaji chema
kinashuka kutoka kwa Baba.

6 Naomba kwa jina la Yesu,
aniombeaye kwake Mungu.
Lolote nitakaloomba
kwa jina lake Bwana anipa.
Sababu hii nakusifu Bwana,
nakushukuru kwa nyimbo zangu.

Text Information
First Line: Nakuimbia wewe Bwana
Title: Nakuimbia wewe Bwana
German Title: Dir, dir, Jehova will ich singen
Author: B. Crasselius
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kumtambikia Mungu: Kumsifu na kumwomba Mungu
Notes: Sauti: Dir, dir, Jehovah will ich singen by B. Crasselius, Asili: Halle, 1704, Posaunen Buch, Erster Band #8, Nyimbo za Kikristo #200
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us