256. Haya ee moyo wangu

1 Haya ee moyo wangu,
imba kwa furaha.
Umwimbie Mwumbaji
mbingu na dunia.
Atukuzwaye pote
umsifu na wewe
kwa nguvu zako zote,
umri wako wote.

2 Mungu wake Yakobo,
ndiye Mungu wetu.
Ukimchagua yeye,
una fungu jema,
unacho kitu chema,
umepata mali;
moyo utakung'aa
shida zitakwisha.

3 Ni mwenye nguvu nyingi,
hana amshindaya.
Kwa hekima aumba,
vyote ni ajabu,
misitu na mabonde,
milima, mashamba,
vilivyo baharini
wanyama porini.

4 Ana mizungu mingi,
kuponya wanawe.
Anawapa riziki,
hata siku za njaa.
Wenye chakula haba
wanenepa miili:
hata waliofungwa
anawafungua.

5 Mashangilio yote,
hayamtoshi yeye.
Ni mwema peke yake
nami ni vumbi tu!
Ananihurumia
kwa kuwa ni wake,
kwa hiyo nalikuza
jina lake pote.

Text Information
First Line: Haya ee moyo wangu
Title: Haya ee moyo wangu
German Title: Du meine Seele, singe
Author: P. Gerhardt, 1607-1676
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kumtambikia Mungu: Kumsifu na kumwomba Mungu
Notes: Sauti: Du meine Seele, singe by J. G. Ebeling, 1666 (Zaburi 146) Posaunen Buch, Zweiter Band #388, Nyimbo za Kikristo #204, Service Book and Hymnal #176 (2nd tune)
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us