163. Kazi Yake Mungu Baba

1 Kazi yake Mungu Baba
imewekwa kwetu.
Kazi yake Mungu Baba
imewekwa kwetu.
Tangu Mwanzo wa Mitume
hadi hivi sasa.
Tangu Mwanzo wa Mitume
hadi hivi sasa.

Refrain:
Na Yeye
Katuagiza
Kasema
Kwa Mamlaka
Aliyo
Pewa na Baba
Nendeni
Duniani pote.
Hubirini kwa Jina la Baba,
Mwana, Roho, watu waokoke.
Hubirini kwa Jina la Baba,
Mwana Roho watu waokoke.

2 Mataifa wana njaa
ya Neno la Mungu.
Mataifa wana njaa
ya Neno la Mungu.
Nayo kiu ya milele
imewakalia.
Nayo kiu ya milele
imewakalia. [Refrain]

3 Hivyo ndugu tutimize
wajibu wa Bwana.
Hivyo ndugu tutimize
wajibu wa Bwana.
Ili siku ikifika
tutoe hesabu.
Ili siku ikifika
tutoe hesabu.[Refrain]

Text Information
First Line: Kazi yake Mungu Baba
Title: Kazi Yake Mungu Baba
Refrain First Line: Na Yeye
Language: Swahili
Publication Date: 1994
Scripture:
Topic: Maisha Ya Kikirsto Na Uhuduma; Wokovu
Notes: Sauti: Mapokeo (Tanzania) Tufurahi na Kuimba #30
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us