Text: | Uliyesulibishwa |
1 Uliyesulibishwa,
Mtakatifu Bwanangu,
uwe ngao shidani,
uniombee mimi.
Uliyesulibishwa,
Mtakatifu Bwanangu!
2 Wongofu sina hata,
niondolee makosa.
Mwovu akinishtaki,
nasumbuka rohoni.
Wongofu sina hata,
niondolee makosa.
3 Wewe tu nipokee,
nakukimbilia wee.
Hata nifanye bidii,
nikatoe machozi.
Wewe tu nipokee,
nakukimbilia wee.
4 Uwe ngao shidani,
niombee na mimi!
Hapa nikiumizwa,
saa ya mwisho ikija:
Uwe ngao shidani,
niombee na mimi!
Text Information | |
---|---|
First Line: | Uliyesulibishwa |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kuteswa na kufa kwa Yesu |
Notes: | Sauti: "Spanish chant," Brosse Missionsharfe, Erster Band #170, Augustana Hymnal #96 |