Text: | Yesu, kuteswa kwako |
Author: | S. V. Birken, 1626-1681 |
1 Yesu, kuteswa kwako
nitakufikiri.
Nipe kwa shauri hili
roho na mbaraka.
Moyo wangu uone
hali yako Yesu,
jinsi ulivyoteswa
kwa ajili yetu.
2 Moyo wangu uone
taabu yako kubwa,
maumivu, mapigo,
na kuwambwa mtini,
taji lako la miiba
tena misumari,
iliyokuumiza,
hata kufa kwako.
3 Nikitazama yote
yaliyokutesa,
nifikiri sababu
na maana yake.
Sababu ndio mimi
na makosa yangu:
umepata mateso,
nipate huruma.
4 Yesu unifundishe
nijute kwa moyo;
nisikuzidishie
shida na uchungu.
Nisiweze kupenda
yaliyokutesa:
nataka kuyaacha
na kukufuata.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Yesu, kuteswa kwako |
Title: | Yesu, kuteswa kwako |
German Title: | Jesu, deine Passion |
Author: | S. V. Birken, 1626-1681 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kuteswa na kufa kwa Yesu |
Notes: | Sauti: Christus, der uns selig macht (patris, sapientia, veritas divina), Asili: Karne 14, Nyimbo za KiKristo; Wimbo: Posaunen Buch, Erste Band #25 |