280. Kwa nini wataka kungoja

1 Kwa nini wataka kungoja?
Ondoka upesi ndugu!
Mwokozi apenda kukupa
pumziko na raha yake.
Mbona? Mbona? Mbona?
hutaki kumjia?
Mbona? Mbona? Mbona
hupendi raha?

2 Ni faida gani kungoja?
Maisha yapita hima.
Ni Yesu tu abarikiye,
kumshika yafaa sana.
Mbona? Mbona? Mbona?
hutaki kumjia?
Mbona? Mbona? Mbona
hupendi raha?

3 Huvutwi moyoni ee ndugu,
na roho yenye uzima?
Hupendi kupata wokovu?
Hima umtafute Yesu.
Mbona? Mbona? Mbona?
hutaki kumjia?
Mbona? Mbona? Mbona
hupendi raha?

4 Kwa nini wataka kungoja?
Kufa kwako ni karibu.
Milango ya mbingu i wazi,
njoo mfuate Yesu Bwana.
Mbona? Mbona? Mbona?
hutaki kumjia?
Mbona? Mbona? Mbona
hupendi raha?

Text Information
First Line: Kwa nini wataka kungoja?
Title: Kwa nini wataka kungoja
English Title: Why do you wait
Author: G. F. Root, 1825-(1820)-1995
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kujuta na kutegemea: Kujuta
Notes: Sauti: Why do you wait by G. F. Root, Reichs Lieder #160, Nyimbo za Kikristo #215
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us