Text: | Mungu upokee moyo wangu |
Author: | J. Rambach, 1693-1735 |
1 Mungu upokee
moyo wangu wote,
niwe mtoto wako,
siku zangu zote.
Nikufuate wewe
nisikuache tena,
nishike siku zote,
ulivyotuagiza.
Unisaidie mimi,
hata kufa kwangu.
2 Msalabani pako,
Yesu naanguka,
uliyenifia
hata mimi pia.
Yaondoe makosa
yatoweke kabisa,
nipate kuwa safi
kwa damu yako bora.
Unisaidie mimi
hata kufa kwangu.
3 Roho Mtakatifu
unanipa nguvu;
niweze kushinda
majaribu yote,
naomba: Utawale
katika moyo wangu,
Shetani hata kufa,
asinishinde mini.
Unisaidie mimi,
hata kufa kwangu.
4 Baba, Mwana, Roho,
uliye mmoje tu,
niliye maskini
nakuomba sana:
Unikubali sasa,
katika ubatizo,
futa makosa yangu
kwa maji haya bora.
Unisaidie mimi,
hata kufa kwangu.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Mungu upokee |
Title: | Mungu upokee moyo wangu |
German Title: | Mein Schöpfer steh mir bei |
Author: | J. Rambach, 1693-1735 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Ubatizo |
Notes: | Sauti: Mein Schöpfer steh mir bei by C. Meyer, 1741, Posaunen Buch #162 |